• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

DAS TABORA AWATAKA WADAU WA MAENDELEO KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI ZA KUPUNGUZA UDUMAVU NA UTAPIAMLO KWA WATOTO HASA MASHULENI

Posted on: September 18th, 2024

Na Alex Siriyako:

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora Bi. Asha Churu kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Deusdedith Katwale amewataka wadau mbali mbali wa maendeleo kama Taasisi Binafsi, Mashirika ya Umma pamoja na Watu Binafasi kujitoa kwa kuwapatia wanafunzi hasa walio na umri wa miaka miatano vyakula vyenye virutubisho kama maziwa, lengo likiwa ni kupambana na udumavu na utapiamlo kwa watoto, hasa wale wa makundi maalumu.

Bi. Churu ametoa wito huu leo Septemba 18, 2024 katika shule ya msingi Furaha, ambayo pia ni shule ya watoto wenye mahitaji maalumu, ambapo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, amezindua program ya kuwapa watoto wa shule hasa za msingi na awali maziwa katika Manispaa ya Tabora ili kupambana na hali ya udumavu na utapiamlo kwa watoto hasa wanaosoma.

Programu hii imezinduliwa leo kwa kuwapatia maziwa yaliyosindikwa watoto wa shule za Furaha, Kizigo na Ipuli, lakini pia program hii kwa awamu hii ya kwanza inalenga kuzifikia shule za msingi na awali kumi na moja (11) zilizopo Manispaa ya Tabora, ambapo chupa 870 zimelengwa kugawiwa kwa watoto katika shule hizo, huku watoto wanaolengwa zaidi wakiwa ni wale waliochini ya miaka mitano pamoja na wale wenye mahitaji maalumu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndugu Elias Kayandabila ameeleza kuwa, mpango wa kuwapatia watoto wa shule maziwa ni utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo amezitaka Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya masuala ya lishe.

Ndugu Kayandabila amefafanua kuwa ziko AFUA ZA LISHE mbalimbali ambazo Halmashauri inatekeleza, hivyo ugawaji wa maziwa ni sehemu tu ya AFUA hizo, ambapo zote kwa pamoja zinalenga kutokomeza kabisa suala la udumavu na utapiamlo kwa watoto hasa walio chini ya miaka mitano, lakini pia na wananchi ambao ni wakubwa wanapaswa kupata milo yenye virutubishi vyote vya msingi katika milo yao ya kila siku.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.