• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA MAALUMU LA MADIWANI MANISPAA YA TABORA LAJADILI RIPOTI YA CAG YA MWAKA WA FEDHA 2019/2020

Posted on: June 16th, 2021

Baraza maalumu la waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya manispaa ya Tabora leo tarehe 16 Juni, 2021, limepata wasaa wa kuijadili na kupata ufafanuzi wa kutosha kuhusu repoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka wa fedha 2019/2020.

 Baraza hilo kiitifaki limehudhuliwa na viongozi mbalimbali kwa nafasi zao ;wakiwemo Katibu Tawala wa Mkoa Tabora Ndg Msalika Makungu, Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Mkoa Ndg Hamu  Mwakasola, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini Mhe. Komanya Erick Kitwala, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora, Katibu Tawala wa Manispaa Tabora Ndg Hammasrsjold Yonaza, waheshimiwa madiwani, wawakilishi wa vyama vya CCM na CHADEMA, wakuu wa Idara na Vitengo mbalimbali, watendaji wa Kata zote pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbal.

Repoti ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ilikuwa na jumla ya hoja 158, ambapo kati ya hoja hizo, hoja 83 ni za miaka ya nyuma na baada ya uhakiki hoja 73 zimepatiwa majibu ya kuridhisha na kufungwa na kusalia na hoja 85 ambazo ni sawa na asilimia 54.

Mkaguzi wa hesabu za serikali Mkoa alieleza kwamba, kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri ya Tabora ilipata hati chafu yaani Adverse Opinion. Na hii ilitokana kwa asilimia kubwa kwa kutokufuata miongozo ya kimataifa ya uandaaji wa hesabu za taasisi za umma yaani IPSAS ambazo kama Nchi tumeridhia kuzifuata.

 Vilevile, Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Mkoa aliendelea kueleza kwamba utekelezaji wa mapendekezo ya Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali sio wa kuridhisha sana na hivyo akaitaka menejiment ya Manispaa ya Tabora ifanye jitihada za dhati kufanyia kazi mapendekezo hayo. Namnukuu.

“Nitoe lai kwa menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kufanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali alisisitiza Mwakasola.”

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa, Ndugu Msalika Makungu alielezea kuwa sehemu kubwa ya chanzo cha kupata hati chafu ni uzembe mkubwa unaofanywa na baadhi ya watumishi wa Manispaa hasa wakuu wa idara, jambo ambalo haliwezi kuendelea kuvumiliwa.

“Hivi jamani hata suala la kupeleka asilimia kumi kwenye vikundi pamoja na kutenga asilimia arobaini kwa ajili ya maendeleo, au  kununua bidhaa na kuweka stoo bila kuingiza kwenye reja pamoja na nyingine nyingi, hizi ni miongoni mwa hoja za kizembe zilizosababisha Halmashauri kupata hati chafu pasipo na sababu za msingi.”

Hivyo akaitaka Menejimenti kubadilika na kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya sita, na kwamba tabia za kizembe kama hizo zinazopelekea Halmashauri kupata hati chafu au yenye mashaka zisijirudie tena.

Aidha kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa Tabora, Mheshimiwa Ramadhani Kapela akihitimisha Baraza kwa kumtaka Mkurugenzi wa Manispaa na Menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kufanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali ili kuweza kufanikisha kufunga hoja zote zilizosalia hususani za mwaka wa fedha 2019/2020. Aliwaasa wakuu wa Idara mbalimbali na watumishi wote wa Manispaa ya Tabora kuwa kitu kimoja na kufanya juhudi kubwa za kuipandisha hadhi zaidi Manispaa na iweze kufikia malengo ya kutoa huduma kwa wananchi wake.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.