• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA MAALUMU LA MADIWANI MANISPAA YA TABORA LAAGIZA KUKATWA FEDHA ZA MISHAHARA KWA WATUMISHI WANAODAIWA

Posted on: August 14th, 2019

Baraza maalumu la Halmashauri ya Manispaa ya Tabora limeazimia  kuwapa wiki mbili Menejimenti ya Halmashauri kuhahakisha inaanza kuwakata kwenye mishahara watumishi wanaodaiwa masurufu yenye thamani ya shilingi milioni 4.7 pesa ambazo zimepelekea kuzalishwa kwa hoja ya Mkaguzi na Mdhiti Mkuu wa Serikali CAG kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Agizo hilo limetolewaleo na Baraza la Madiwani Manispaa ya Tabora baada ya kupokea pendekezo la Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa Kikao Maalumu cha Baraza la Madiwani ya kupitia hoja ya mbalimbali kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2017/18.

Madiwani walikubaliana kwa kauli moja kwamba ndani ya wiki watumishi wote wanaodaiwa wahakikishe wamelipa fedha hizo au wakatwe kwenye mishahara yao.

Walisisitiza kwamba iwapo wasipokatwa fedha hizo hoja hiyo itaendelea kujitokeza na hivyo itapelekea muendelezo wa kuchafua hesabu za Manispaa ya Tabora na heshima yake pia.

Pamoja na hilo Baraza la Madiwani pia lilikubaliana na agizo la Mkuu wa Mkoa huyo ambalo linawataka Wakuu wa Idara kuhakikisha wamefanyia kazi hoja zote za CAG ndani ya wiki mbili tuu na kuwalisilisha vielelezo vyote ili hoja ziweze kufungwa .

Mkuu wa Idara ambaye ndani ya kipindi hicho atashindwa kujibu hoja hizo na kusababisha kuendelea kuwepo atachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kuondolewa katika nafasi yake, alisema Mwanri.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tabora amewataka uongozi wa Manispaa ya Tabora kuhakikisha wanakusanya madeni yote ya ardhi na mikopo ya wanawake, vijana na walemavu yanayo kadiriwa kufikia zaidi ya milioni 536.

Kumekuwepo na uuzaji wa viwanja vya Halmashauri ambapo wananchi waliotakiwa kufidiwa maeneo yao hawakulipwa mpaka sasa na wale ambao walipewa viwanja wamekuwa wakilipa kidogo kidogo na hivyo kusababisha deni kuwa kubwa la kufikia zaidi ya milioni 503, na hivyo akawataka kushughurikia hilo nalo liondolewe kwenye vitabu vya CAG, alisema Mwanri.

Pia Mwanri alitumia fulsa hiyo kusisitiza ufuatiliwaji na urejeshwaji wa fedha za vikundi vya wanawake, vijana na walemavu ipatayo milioni 33.7 irejeshwe haraka ili na wengine waweze kukopeshwa.

Awali Mkuu waWilaya ya Tabora Komanya Kitwala alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa kuhakikisha kuwa anawachukulia hatua watumishi wote ambao wameisababishia Halmashauri kuzalisha hoja za kiukaguzi. Pia alisisitiza kuwepo na kuwajibishana, kutunza kumbukumbu na mwisho kuwepo na uthubutu kwa Mkurugenzi.

Watumishi wanapaswa kujitahidi kuzuia hoja zisitokee na siyo kupelekea maamuzi ambayo yanasababisha kuendelea kwa uzalishwaji wa hoja kila mwaka alisema Komanya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.