• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA USHAURI WILAYA YA TABORA (DCC) LAPITISHA RASIMU YA BAJETI 2022/2023 PAMOJA NA MAPENDEKEZO YAKE

Posted on: January 7th, 2022

Na Paul Kasembo-TMC.

Baraza la Ushauri Wilaya ya Tabora lajadili na kupitisha Rasimu ya Bajeti 2022/2023 pamoja na mapendekezo yake yenye lengo la kuboresha na kuleta tija kwa muktadha mpana wa wananchi wa Wilaya ya Tabora.

Akifungua Mkutano wa Baraza, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda, alianza kwa kuwaeleza wajumbe juu ya Mapitio ya Bajeti iliyokwisha kwa mwaka wa fedha 2020/2021kwamba kumekuwa na mafanikio makubwa sana katika utekelezaji wa maazimio ya Baraza lenyewe.

Ambapo Manispaa katika utekelezaji wa yatokanayo na Mkutano wa mwakwa wa fedha 2021/2022 imeweza kufautilia vifaa vya na fedha zilizotolewa na wadau mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya , ambapo mrejesho wake ni kwamba vifaa hivyo vilitumika kwenye ujenzi wa Ofisi za Kata.

Aidha fedha kwa ajili ya ukarabati wa Ukumbi wa Taasisi (Sanamu ya Mwl Nyerere) kiasi cha zaidi ya Tzs Mil.90 zilitemetengwa, pamoja na kufanya mchakato wa upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuweka vitega uchumi (Maduka) kuzunguuka Uwanja wa Vita unaendelea.

Akisoma taarifa ya makadirio ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nawanda alisema kuwa, Manispaa ya Tabora imekusudia kufuata misingi itakayozingatia kufikia shabaha za ukusanyaji mapato.

Ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa ushiriki wa Sekta binafsi kwenye shughuri za maendeleo, kuimarika kwa uchumi wa Taifa, kuendelea kuwa na utosherevu na upatiakanaji wa chakula ndani ya Manispaa , uwepo wa amani, usalama na utulivu miongoni mwa wananchi wa Manispaa ya Tabora.

Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Manispaa imepanga kuwa na vipaumbele vingi vyenye tija vikiwamo;

 Kuongeza ukusanyaji wa mapato kwa kubuni vyanzo vingine vipya 9, kujenga stendi ya kisasa katika eneo la Inala, kujenga stendi ya malori katika barabara zinazounganisha Njia kuu za Mikoani kuja stendi ya Inala.

kujenga hosteli ya wanafunzi, kujenga shopping mall mbili za kisasa zaidi, kuboresha eneo la PPP Kitete kwa ajili ya kujenga vibanda vya biashara vvyenye ghorofa, kuanzisha maegesho ya magari madogo katikati ya mji.

Sambamba na kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kutumia teknolojia ya TEHAMA, kuongeza fedha kwa ajili ya miundombinu ya Sekta za Afya, na Elimu, kuwezesha wananchi kiuchumi kwa kutoa mikopo kwa vikundi vya wajasiliamali kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Kando na hayo, pia Manispaa imejipanga kutekeleza mpango wa Bajeti yake kwa kuzingatia mikakati kama ifuatavyo; kukamilisha Miradi viporo ikiwamo jengo la Utawala , Hospitali ya Wilaya , Miundombinu ya Elimu na Afya,

Ulipaji wa fidia kwa wananchi kwa  ajili ya kutatua migogoro mbalimbali na kutwaa maeneo ya uwekazaji wa viwanja, kudhibiti utoroshaji wa mazao ya kilimo na misitu kwa kuendelea kuweka vizuizi katika njia ambazo hutumika na wafanyabiashara.

Pamoja na kuingia mikataba na wakusanyaji wa mapato katika vyanzo vyote ili wawepo muda wote wa kukusanya mapato, kuhamasisha jamii kuchangia miradi ya maendeleo pamoja na kutoa elimu kwa wafanyabiashara waone umuhimu wa kulipa kodi.

“Katika hili naomba nitoe wito kwa Wadau wa Maendeleo katika Manispaa ya Tabora wakiwamo wafanyakazi, wafanyabiashara, Waheshimiwa Madiwani na Taasisi zisizo za Kiserikali waweze kushiriki kikamilifu kwenye kuchangia shughuri na utekelezaji wa Bajeti hii ili juweza kufikia malengo yaliyo tajwa”, alisema Dkt. Nyanja.

Kwa upande wake Mstahiki Meya Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela, alimshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu kwa namna ambavyo anaendesha Nchi, na kuipatia fedha nyingi Manispaa ya Tabora ambazo zimejenga miundombinu ya Elimu na Afya.

Aidha Meya akampongeza Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Waheshimiwa Madiwani, Mkurugenzi na wataalamu wa Manispaa kkwa namna ambavyo wanachapa kazi nzuri, n kwamba wana nia njema sana Manispaa ya kuivusha kuja kuwa Jiji.

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imeomba kuidhinishiwa fedh jumla ya Shilingi 44,954,619,932.16 ambapo kati ya fedha hizo Tzs 10,626,677,093.24 ni Ruzuku ya miradi ya maendeleo kutoka Serikali Kuu, Tzs 25,415,574,012.00 ni fedha za Mishahara.

Aidha Tzs 5,451,254,158.25 ni fedha za Mapato ya  Ndani (mapato halisi Tzs 4,781,615.100 na mapato fungwa Tzs 669,639,058.25) ambayo imeidhinishwa na Baraza la Ushauri Wilaya ya Tabora.

 

 

 

MWISHO 

Matangazo

  • ORODHA YA WAOMBAJI WALIOTEULIWA KATIKA AJIRA ZA MUDA ZA SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 July 28, 2022
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA TULI KATA YA IFUCHA - INALA July 25, 2022
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Usafi wa Mazingira kwa Wananchi Wote, Jumamosi ya mwisho kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA NNE KWA MWAKA 2021/2022 LAIPINGEZA MENEJIMENTI

    July 30, 2022
  • UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA USHIRIKA DUNIANI YAFANYIKA TABORA

    June 28, 2022
  • MANISPAA YA TABORA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA 2020/2021

    June 22, 2022
  • MKUU WA WILAYA AWAHAKIKISHIA USALAMA WATOTO WOTE WA MANISPAA YA TABORA

    June 16, 2022
  • Angalia Zote

Video

MSTAHIKI MEYA BW. RAMADHAN KAPELA - UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NA UWEKEZAJI KATIKA MANISPAA YA TABORA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA
  • Taarifa Mbalimbali
  • Fomu ya maombi ya Leseni
  • Jarida 2020
  • eMrejesho
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Manispaa Tabora, 4 Barabara ya Kiwanja cha Ndege

    Anwani ya Posta: S.L.P 174, 45182 Tabora

    Simu ya Ofisi: 026-2604315/6088

    Simu ya Mkononi: 0784705044

    Barua Pepe: md@taboramc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.