• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA MADIWANI ROBO YA NNE KWA MWAKA 2021/2022 LAIPINGEZA MENEJIMENTI

Posted on: July 30th, 2022

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Tabora robo ya nne limeipongeza Menejimenti na Mkurugenzi wa Manispaa kwa kutekeleza vema wajibu na majukumu yao na hata kuiwezesha Manispaa ya Tabora kupata Hati Safi kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Akitoa pongezi hizo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Shabani Kapela aliwaeleza wajumbe wa baraza kuwa, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora pamoja na Menejimenti yake wamefanya kazi nzuri sana ya kujituma kukusanya mapato hata sasa tumeweza kupata asilimia 94 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 tofauti na kipindi cha miaka ya nyuma ambapo hatukuwa tukifikia asilimia hizo.

“Kipekee kabisa baraza la madiwani likiongozwa na mimi mwenyewe Mstahiki Meya, tunatoa pongeza za dhati kwa Mkurugenzi wetu Dkt. Peter Nyanja na Menejimenti yake kwa kuweza kukusanya mapato makubwa na hata kufikia asilimia 94, tofauti kubwa tunaiona hivi sasa inatokana na Mkurugenzi wetu akisaidiwa na Menejimenti yake mfenya kazi nzuri sana tunawapongeza,” alisema Mstahiki Meya Kapela.

Aidha Mstahiki Meya alitumia fulsa hiyo kumshukuru sana Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna ambavyo anliletea maendeleo Taifa la Tanzania na kuwaunganisha watu wake. Kisha akampongeza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi. Dkt. Batilda Burian kwa nama ambavyo amekuwa akiwatumikia wananchi wa Mkoa wa Tabora na Wilaya zake zote.

Pongezi za kipekee kwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Esmail Nawanda kwa utumishi wake bora ulipelekea hata Mhe. Rais akaiona na kuamua kumpandisha cheo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, hakika ni furaha kubwa sana kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora kwakuwa kupanda kwake kumetokea katika eneo ambalo wananchi walikuwa wakimpenda sana.

Akitoa shukurani zake Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda aliwashukuru sana waheshimiwa madiwani wa Manispaa ya Tabora wakiongozwa na Mstahiki Meya Mhe. Kapela na wananchi wa Manispaa ya Tabora kwa namna ambavyo walikuwa wakisapoti katika kazi zake za kila siku katika kuwatumikia wananchi wa Manispaa ya Tabora tangu kufika kwake.

“Niwashukuru sana Waheshimiwa Madiwani wangu mkiongozwa na Mstahiki Meya wetu kwa namna ambavyo mmekuwa msaada mkubwa kwangu katika kutekeleza majukumu yangu ya kila siku nikiwa hapa kama Mkuu wa Wilaya, hakika nitawakumbuka sana na wala sijutii kufanya kazi hapa,” alisema Dkt. Nawanda.

Katika hatua nyingine Dkt. Nawanda aliwaomba waheshimiwa madiwani na menejimenti kwenda kuendeleza miradi waliyokuwa wameianzisha ili ije kuwa na tija kwa wananchi wa Manispaa na vizazi vijavyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Maiga Nyanja aliwashukuru sana Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuikumbuka Manispaa ya Tabora na hata kuiongezea fedha katika miradi mbalimbali, Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa kuendelea kumsapoti kwenye kazi zake za kila siku, Mkuu wa Wailaya ya Tabora kwa kukubali kufanya kazi bega kwa bega hata kuweza kufikia malengo ya Manispaa katika kukusanya mapato, Mstahiki Meya kwa ushirikiano mkubwa anaompatia wakati wote wakati wa kutekeleza majukumu yake, wahe. Madiwani na watumishi na wadau wote kwa ujumla.

“Kwangu mimi nyote ni watu muhimu san katika kuniwezesha kutekeleza majukumu yangu ya kila siku, binafisi nafarijika sana na menejimenti yangu inaungana nanyi kwenye kila maelekezo mnayotoa na mtakayoendelea kuyatoa yatatekelezwa kama mtavyoelekeza kwa asilimia mia moja, nawashukuruni sna hata kwa kuikubali Taarifa yangu ya Utekelezaji na Uwajibikaji ya mwaka fedha 2021/2022,” alisisitiza Dkt. Nynaja.

Kando na hayo, baraza pia lilifanya uchaguzi mdogo wa kumpata Naibu Meya wa Manispaa ya Tabora ambapo Mhe. Nassir I. Mnenge alifanikwa kuibua mshindi na hivyo kuwa Naibu Meya ambaye atahudumu kwa kipindi cha mwaka 2022/2023 akimrithi Mhe. Kasongo Amrani ambaye alihudumu kwa vipindi viwili mfululizo.

Kukamilika kwa baraza hili la mwaka wa fedha 2021/2022, kunafungua ukurasa mpya wa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo Manispaa ya Tabora ikiwa na malengo pamoja na mikakati mipya katika kukusanya mapato na kuwahudumia wananchi wake wa Manispaa ya Tabora.

 MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.