• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA MADIWANI LAMPONGEZA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TABORA KWA KASI YAKE YA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: November 3rd, 2022

Na Alex Sriyako-TMC

Wajumbe wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela wametoa pongezi zao za dhati kabisa kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter M. Nyanja na Menejimenti yote kwa ujumla kwa kasi yake ya ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ambapo kwa kipindi cha Julai-Septemba 2022/2023 Halmashauri imekusanya asilimia 32.15, na mpaka kikao cha robo ya kwanza kinafanyika mnamo tarehe 2.11.2022 makusanyo yako asilimia 43.59, kasi amabayo inaridhisha sana.

Wajumbe wa Baraza wamempongeza Mkurugenzi na kuongeza kuwa kwa Manispaa ya Tabora kwa miaka ya hivi karibuni hawajawahi kuona kasi ya ukusanyaji wa mapato kwa kiwango hiki. Wajumbe wamesisitiza jitihada hizi za makusanyo ni za kuungwa mkono kwa nguvu zote kwani uhai wa Halmashauri ni mapato.

Aidha Mstahiki Meya katika hotuba yake ya ufunguzi amemshukuru sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi sana za miradi katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora hususani Sekta ya Elimu ambayo ndiyo roho ya uchumi endelevu wa Taifa, na akakumbusha tu kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba miongoni mwa fedha sekta ya Elimu imepokea, Halmashauri imepokea kiasi cha Bilioni moja ,milioni miatatu na themanini (1,380,000,000) kwaajili ya ujenzi wa madarasa ya wanafunzi wa kidato cha kwanza.

Wakati huohuo, Wajumbe wa Baraza wametoa tuzo ya Ngao kwa Wananchi wawili wa Manispaa ya Tabora kwa kuonyesha uzalendo mkubwa na wa kuigwa wa kutoa maeneo yao kupisha ujenzi wa miundombinu ya Elimu. Wananchi hao ni Mhe. Mohamed Katete, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora ambaye ametoa eneo lake ili ijengwe Shule ya Msingi katika Kata ya Ipuli, pamoja na Ndugu Idd Rajabu ambae ametoa eneo ilipojengwa Shule ya Sekondari Mpera, kata ya Mpera. Wajumbe waliongeza msisitizo kuwa Shule ya Msingi inayojengwa isajiliwe kwa jina la Mzee Katete ili kuenzi mchango wake katika jamii na kwa upande wa Ndugu Rajabu apewe jina la Mtaa kwasababu Shule ya Mpera imeshasajiliwa kwa jina tofauti.

Katika Baraza hili vilevile kumeibuka hoja za utekelezaji usiolizisha wa Shirika la Umeme Nchini(Tanesco) Mkoa wa Tabora hususani kwenye kasi yao ya kupeleka umeme vijijini. Hata hivyo wajumbe wameishia kumuagiza mwakilishi wa Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tabora baada ya Meneja kuwa na udhuru na kushindwa kuhudhuria Baraza hili. Aidha Wajumbe wameliomba Shirika la Umeme Mkoani Tabora lirudishe umeme katika chanzo cha Uzalishaji wa Maji cha Mto Igombe ambacho kipo chini ya Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mkoani Tabora (TUWASA) ili Wananchi waendelee kupata huduma ya maji na kuongeza kuwa changamoto zingine zitatuliwe kiofisi.

Msathiki Meya wa Manispaa ya Tabora katika kuhitimisha Baraza hili amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kuendeleza kasi yake ya kukusanya mapato kwa kushirikiana na wadau wake wote na ajitahidi kusikiliza kero zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.