• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA MADIWANI LAADHIMIA KUPANDISHA MAPATO

Posted on: August 26th, 2021

Mheshimiwa Ramadhani Kapela, ambae ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, ameongoza kikao cha Baraza  la Waheshimiwa Madiwani cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2020/2021.

Baraza hilo vilevile limehudhuriwa na viongozi mbalimbali, akiwemo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM), Wilaya ya Tabora, Ndg.Mohamed Katete, Mkuu wa wilaya ya Tabora, Dkt. Yahaya Nawanda, Mkurugezi  wa Manispaa ya Tabora,Dkt Peter Nyanja, Katibu tawala wa Wilaya ya Tabora, Ndg.Hamarskjold Yonaza, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora, Ndg. Sefu Salum,Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Waheshimiwa madiwani, Watendaji wa serikali, pamoja na  wageni waalikwa.

Mstahiki Meya alifungua kikao hicho mahususi kwa ajili ya maamuzi na ustawi wa maendeleo ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora na aliwakaribisha Mkuu wa wilaya Yahya Ismail Nawanda katika baraza lake la kwanza na Mkurugezi mpya Dkt Peter Maiga Nyanja. Alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt Batilda Burian, kwa kazi zake nzuri na alimshukuru  Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu kwa uongozi wake mzuri na  vilevile alishukuru kwa ushirikiano anaopata kutoka kwa madiwani.

Mheshimiwa Ramadhani alisisitiza hatua za dhati zichukuliwe kuinua mapato, asilimia za maendeleo kutoka kwenye makusanyo ziende kwa wananchi kwa wakati, na zaidi ya yote akasisitiza viongozi wa serikali lazima wawe mstari wa mbele kuhamasisha zoezi la chanjo za UVIKO-19.

Dkt.Peter Nyanja, yeye aliomba ushirikiano kutoka kwa madiwani pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama hususani kwenye kazi kubwa ya ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri, kwani anaamini kuna uwezekano mkubwa wa kufikia asilimia mia moja, ikiwa ni pamoja na kusuluhisha matatizo madogo madogo ya ulipaji kodi, pia aliomba kuungwa mkono katika uimarishaji wa usafi wa mji na kusisitiza biashara holela zipigwe marufuku kwamba kila biashara ina sehemu yake stahiki na kodi stahiki za Halmashauri lazima zilipwe.

Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Dkt.Yahaya Nawanda, naye alipata fursa ya kuzungumza machache, ambapo alimshukuru Rais kwa kuendelea kumuamini katika nafasi hiyo, aliahidi ushirikiano mkubwa sana kutoka kwa Kamati yake ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya. Alisema hatokubali Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kuwa ya mwisho kwenye mapato, na zaidi ya yote alitoa rai kwa matumizi sahihi ya fedha zinazokusanya, ikiwa ni sambamba na uwepo wa nyaraka zote za manunuzi, na matumizi mengineyo.

Miongoni mwa matukio yaliyofanyika ndani ya vikao hivi ni pamoja na kuzitambua na kuzitunuku vyeti shule za Msingi na Sekondari za Tabora Manispaa, zilizofanya vizuri katika mitihani ya Taifa kwa mwaka 2020, Kumtambua na  kumpongeza mwanafunzi Bora Hassan wa Shule ya Sekondari Nyamwezi kwa kutwaa nishani nne katika michuano ya UMISETA ngazi ya Taifa. Hali kadhalika, Baraza limepokea ripoti ya Mpango kazi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kutoka Shirika la umeme TANESCO, pamoja na TARURA

Baraza vilevile ndani ya vikao vyake vya siku mbili limeweza kupata fursa ya kuuliza maswali ya papo kwa papo kwa Meya, limepokea taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kila kata, limepokea Mihutasari na maadhimio ya Kamati mbalimbali za kudumu, Lakini vilevile Baraza limepokea taarifa ya Mkaguzi wa Ndani kwa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2020/2021.

Kabla ya kufunga kikao, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tabora, Ndg. Mohamed Katete, alimpongeza mwenyekiti wa kikao, Mh.Ramadhani Kapela kwa kuonyesha umahiri wake na kuweza kuwaunganisha Watendaji wa Serikali na Waheshimiwa  Madiwani. Hali kadhalika, Ndg.Katete alisema kwamba Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ina mipango mingi mikubwa ila haijatekelezwa kwa sababu ya changamoto kama vile ukosefu wa uadilifu na uwajibikaji, hivyo aliwaasa viongozi kubadirika na kufanya kazi kwa bidii na kuwa wavumilivu na kuwa watunzaji wa kumbukumbu na nyaraka muhimu za Serikali.

Mwenyekiti wa kikao ambae ni Meya wa Manispaa ya Tabora, Mh. Ramadhani Kapela alifunga kikao hicho  kwa kumshuru Mungu kwa uzima, uhai, hekima na busara kwa kumaliza kikao hicho salama, pia alishukuru kwa ushirikiano mkubwa kutoka Waheshimiwa Madiwani. Hali kadhalika, Meya alisisitiza Viongozi wa Serikali kuwa mstari wa mbele kuhamasisha chanjo, na alitanabaisha kwa mara nyingine kwamba kipaumbele cha Baraza la Madiwani ni kuongeza Mapato kadri itakavyowezekana.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.