• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

ANAISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI KWA ZAIDI YA MIAKA KUMI NA SITA SASA

Posted on: December 2nd, 2021

Na Alex Siriyako,

Mzee Joseph Rutambuka mwenye umri wa miaka 65 mpaka sasa, ni mkazi wa Kata ya Mtendeni iliyopo manispaa ya Tabora,ambae mpaka sasa ameweza kuishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa zaidi ya miaka kumi na sita . Mzee Rutambuka alibainika na maambukizi ya VVU kwa mara ya kwanza mwaka 2005.Anaeleza kuwa siri ya mafanikio yake ni matumizi mazuri ya dawa za kupunguza makari ya Virusi pamoja na kufuata ushauri mwingine wa madaktari kama kula vizuri,kuepuka ngono uzembe,kufanya mazoezi pamoja na kujiamini na kuwa mwenye furaha muda mwingi.

Mzee Joseph Rutambuka ni miongoni mwa mashujaa wa siku ya UKIMWI DUNIANI,kwani ni miongoni mwa waathirika wachache sana Nchini Tanzania ambao wamejitokeza hadharani na kuieleza jamii kwamba wao ni wahanga wa VVU.Mzee anaishi na maambukizi na sasa amekuja kuwaelimisha wakazi wa Itulu,na kuwatia moyo wale wenye maambukizi kwamba wasikate tama kwani inawezekana kuishi na maambukizi na ukafikia ndoto zako.

Pamoja na mafanikio hayo vilevile Mzee Rutambuka anaeleza changamoto ambazo amekutana nazo ikiwa ni pamoja na kupoteza wanafamilia ambao ni mke na mtoto mmoja. Vilevile amenyanyapaliwa sana na jamii pindi alipobainika anamaambukizi ya UKIMWI. Lakini amepambana na changamoto hizo na anawaasa wanajamii waweze kuchukua hatua dhidi ya gonjwa hili ikiwa ni pamoja na kupima mara kwa mara ,Kuchukua dawa za kupunguza makari ya Virusi mapema pindi wanapobainika kuwa na VVU ,pamoja na kuwapenda wenye VVU na kuwafariji badala ya kuwanyanyapaa.

Katika maadhimisho hayo ya siku ya UKIMWI DUNIANI ambayo kitaifa yaliadhimishwa Mkoani Mbeya, kwa Wilaya ya Tabora yalifanyika kijiji cha Itulu,kata ya Ndevelwa. Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mh.Dkt.Ismail Yahaya Nawanda ambae alipata wasaa wa kuongea na Wananchi wa Itulu. Dkt.Nawanda alieleza vizuri kuwa malengo mahsusi ya Siku ya UKIMWI Duniani ni kuwakumbuka wapendwa waliotutoka kwa sababu ya janga hili,lakini pia ni kupata fursa ya kukumbushana kuwa UKIMWI bado upo na unaendelea kututafuna taratibu na hivyo hatuna budi kuendelea kuchukua hatua madhubuti za kuendelea kupambana ili hatimae tuweze kulitokomeza janga hili.

Dkt.Nawanda ameeleza mikakati ya Serikali katika kupambana na janga hili ni pamoja na kuhakikisha maambukizi mapya ya VVU yanafikia sifuri,Unyanyapaa kwa watu wanaoishi na VVU unakwisha, pamoja na kuhakikisha kwamba vifo vitokanavyo na UKIMWI vinakwisha kwa kuendelea kutoa elimu kwa wadau wote.

Lakini pia Mkuu wa Wilaya alitoa wito kwa Wananchi kijitokeza kupima kwa hiari ili kujua afya zao, akinababa waende na kina mama kiliniki ili kujua afya zao na kuweza kumkinga mtoto na maambukizi ya VVU. Pia alitoa wito kwa wadau kupata chanjo ya UVIKO-19, kwani CORONA ipo na inaua,njia pekee ya mwisho kukabiliana nayo kwa sasa ni chanjo. Dkt.Nawanda alimaliza kwa kusema “Tabora Manispaa bila maambukizi mapya ya UKIMWI inawezekana”

Bi.Aziza Mageta,ambae ni Mratibu wa UKIMWI katika Manispaa ya Tabora,katika risala yake fupi ameeleza Historia ya Gonjwa la UKIMWI kwa ufupi sana. Ameeleza kuwa ugonjwa huu uligundulika kwa mara ya kwanza Nchini Marekani mnamo mwaka 1981,na kwa Tanzania ugonjwa huu ulionekana Mkoani Kagera mwaka 1983, na mnamo mwaka 1984 ugonjwa huu ulikuwa umeingia Mkoani Tabora. Alieleza pia mnamo mwaka 1985 mgonjwa wa kwanza alilipotiwa ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

Lakini vilevile Bi.Aziza ameeleza namna ambavyo wakazi wa Tabora wanahitaji kuchukua tahadhari zaidi kwani hali ya maambukizi kwa Wilaya yetu sio nzuri, kwani kwa mwaka 2019/2020 kiwango cha maambukizi kilikuwa 3.5, na kwa mwaka 2020/2021 kiwango cha maambukizi ni 3.8 hali ambayo ni ya hatari sana kwani maambuklizi yameeongezeka kwa asilimia tatu(3%). Hivyo amewaomba Wananchi wote wa Tabora tutambue hali hii na tuongeze jitihada katika kupambana na janga hili.

Miongoni mwa wadau waliofika katika kuadhimisha siku hii ya UKIMWI DUNIANI katika Kijiji cha Itulu,Kata ya Ndevelwa Wilayani Tabora ni pamoja na DAMU SALAMA kanda ya Magharibi,EWURA-CCC, Shirika risilo la Kiserikali la COMPASSION, Mpango wa TOHARA, pamoja na Wataalamu wa Wizara ya Afya wa Chanjo ya UVIKO-19, na Upimaji wa VVU. Vilevile Wananchi wa kata ya Ndevelwa walihudhuria kwa wingi wao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.