• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI UMMY APIGA MARUFUKU MICHANGO MASHULENI

Posted on: December 16th, 2021

Na Alex Siriyako,

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Raisi,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mh.Ummy Mwalimu amepiga marufuku michango yeyote isiyofuata utaratibu katika shule zote za Sekondari na Msingi.Waziri Ummy ametoa onyo hili katika ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora,katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Na katika msisitizo wa onyo hilo,Waziri ametoa Salamu za Mh.Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suruhu Hassani kwa WanaTabora,kwamba Mh.Raisi ataendelea kutoa fedha za Elimu bure, hivyo Wananchi wapuuze taarifa zinazosambaa za kulipa ada Mashuleni.

Waziri Ummy amekagua Miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora. Miongoni mwa miradi aliyopata fursa ya kutembelea na kukagua ni pamoja na; Ujenzi wa Madarasa mawili na Ofisi moja katika Shule ya Sekondari Kariakoo. Mh.Ummy ameridhika na ubora wa madarasa na kwa kuthibitisha hilo ameahidi kuleta milioni hamsini(50,000,000/=) za kujenga Jengo la Utawala shule ya Sekondari Kariakoo.Lakini vilevile alitumia wasaa huo kukanya na kuonya juu ya michango isiyofuata taratibu za kisheria na kusema kwamba michango yote ya shule kwanza lazima ijadiliwe na kukubaliwa na bodi ya shule kabla ya Vyombo vingine vya Serikali.

Mh.Ummy aliweza kukagua Kikundi cha Vijana cha Miombo Bee Keepers Initiatives, Kikundi cha Vijana kinachojihusisha na Ufugaji Nyuki na Kusindika Mazao ya Nyuki.Kikundi hiki ni miongoni mwa Vikundi vilivyopata mkopo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mkopo wa kiasi cha shilingi Milioni Hamsini(50,000,000/=),ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Raisi kwa Halmashauri zote Nchini kutoa mikopo yenye tija kwenye vikundi vya wajasiriamali,badala ya mikopo ya pesa ndogo ndogo,ambayo haiwainui  vijana ipasavyo.

Halikadhalika Mh.Ummy amekagua Ujenzi wa Haspitali ya Wilaya ya Tabora,ambapo ameridhika na ubora wa Majengo lakini pia ametoa maagizo Halmashauri ifanye hima iweze kumaliza ujenzi huo ili Wananchi waanze kupata huduma, vile vile amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Dr.Peter Nyanja,aanze kujenga nyumba za watumishi kwa mapato ya ndani.

Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI amekagua ujenzi wa Barabara ya Milambo Barracks, barabara yenye urefu wa Mita mia nane inayojengwa kwa kiwango cha rami kwa kutumia fedha za Serikali na inatarajia kugharimu kiasi cha shilingi milioni miatatu ishirini  mpaka kukamilika.Mh.Ummy ameridhika na kasi ya ujenzi na kuhimiza mradi umalizike kwa wakati.

Waziri Ummy anaendele na Ziara yake Mkoani Tabora, kwa Upande wa Halmashauri ya Manispaa yaTabora ,amempongeza kwanza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Batilda Buriani, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Dkt.Yahaya Nawanda pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa usimamizi wao mzuri wa miradi ya maendeleo hususani utekelezaji wa ujenzi wa madarasa 74 ya Mpango wa Taifa wa Ustawi na Mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.