• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WATAALMU WA MANISPAA YA TABORA WASAINISHWA MIKATABA YA KUKUSANYA MAPATO

Posted on: July 10th, 2023

Na Alex Siriyako;

Wataalamu wa Manispaa ya Tabora ambao ni Wakuu wa Divisheni na Vitengo wenye kusimamia vyanzo vya Mapato wamesainishwa Mikataba ya kuhakikisha kuwa wanafikia malengo ya ukusanywaji wa mapato katika vyanzo wanavyovisimamia  kwa asilimia mia moja ama zaidi kwa kadri ya makisio ya bajeti ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2023/2024 kwa mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mikataba hiyo imesainiwa leo Julai 10,2023 baina ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndugu Elias M. Kayandabila na Wakuu wa Sehemu na Vitengo wenye Vyanzo vya Mapato ambavyo wanavisimamia katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora huku zoezi hili likishuhudiwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela.

Akieleza kikao kabla ya utiaji saini huu, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora ameeleza kuwa Bajeti ya Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ni bilioni 6.15 ambazo zinatokana na vyanzo vingi ambavyo vinasimamiwa na Wakuu wa Sehemu na Vitengo tofauti tofauti.

Mkurugenzi ameongeza kuwa ili kufanikisha zoezi la kukusanya Mapato ya ndani kwa ufanisi, Wakuu wa Sehemu na Vitengo hawana budi kusimamia vyema na kwa weledi na uaminifu vyanzo vilivyo chini yao na kuhakikisha kuwa makisio waliyokadiria kwenye vyanzo hivyo yanakusanywa ipasavyo.

Nae Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela kwa nafasi yake amempongeza Mkurugenzi kwa jitihada zake za awali za kuhakikisha kuwa mapato ya Halmashauri yanapatikana kwani mapato ndio roho ya Halmashauri yeyote ile Duniani.

Mhe. Kapela ameongeza kuwa ana imani kubwa sana na Wakuu wa Sehemu na Vitengo waliopo kwani kwa miaka miwili ya fedha iliyopita wamefanya kazi nzuri ya makusanyo ya mapato ya ndani ikiwa ni sambamba na kuzifanyia kazi hoja za ukaguzi na kupata hati safi kwa miaka miwili hiyo mfululizo.

Hivyo Mstahiki Meya amewataka Wakuu wa Sehemu na Vitengo wasiwe na wasiwasi na Mikataba hii kwani ina lengo zuri sana la kuongeza tija na ufanisi kwa mtu mmoja mmoja kama Kiongozi katika usimamizi wa chanzo ama vyanzo vilivyo chini yake na ameongeza kuwa atafurahi sana kama kutakuwa na bonasi kwa Mkuu wa Sehemu ama Kitengo atakaye kusanya zaidi ya asilimia mia moja.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.