• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

NIWATAKE AJENDA YA LISHE IWE YA KUDUMU KATIKA VIKAO VYENU

Posted on: October 28th, 2022

Na Alex Siriyako,

Haya yamesemwa na Bi. Haika Masue, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora akimuwakilisha Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Paul Chacha katika kikao cha tathimini ya lishe Manispaa ya Tabora kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa leo tarehe ishirini na nane Oktoba.

Manispaa ya Tabora kupitia kwa Watendaji wake kama Maafisa Lishe na Watendaji Kata, inayo dhima na dhamana kubwa sana kuhakikisha kuwa Wananchi wake wanapata lishe bora na yenye virutubisho vyote muhimu kwa afya zao.

Bi. Haika amesisitiza kuwa Lishe duni sio tu inaathiri maendeleo ya mtoto lakini pia inaathiri ukuaji wake kimwili na kiakili na hatimaye kuathiri mchango wake katika maendeleo ya Taifa kipindi chote cha uhai wake.

Ametanabaisha kuwa hali ya Utapiamlo katika Mkoa wa Tabora ni kubwa hali ambayo ni mbaya Zaidi kwa watoto chini ya miaka mitano, wanawake wajawazito na akina mama wanaonyonyesha. Hali kadhalika amewaasa Wakazi wa Tabora kunawa mikono kwani afya bora huanzia kwenye usafi wa mwili ikiwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara.

Bi. Haika amewakumbusha Menejimenti ya Manispaa ya Tabora kuwa mnamo tarehe 30/9/2022 Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ameingia Mkataba na Wakuu wa Mikoa yote Nchini ya uboreshaji wa shughuli za Lishe, Mkataba utakaodumu kwa miaka minne na umeainisha vipaumbele vyake pamoja na viashiria vya lishe. Hivyo Manispaa ya Tabora  ina dhima na dhamana kubwa  kufanya vizuri sana  katika kutekeleza mkataba huu.

Hali kadhalika Wajumbe wa kikao hiki wakiongozwa na muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tabora walishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Lishe baina ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora na Watendaji wa Kata 29 za Manispaa ya Tabora. Ambapo kwa mkataba huo, Watendaji Kata watahakikisha Wananchi kwenye Kata zao wanapata Vyakula vyenye virutubisho vyote muhimu ili kuepuka utapiamlo.

Ndugu Sefu Salumu Sefu, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora naye amepata wasaa wa kuzungumza na wajumbe ambapo amepokea maelekezo yote ya Serikali na kusisitiza kuwa Menejimenti ya Manispaa ya Tabora ikiongozwa na Mkurugenzi wake itahakikisha mikataba ya lishe baina ya Mkurugenzi na Watendaji wa Kata inatekelezwa kwa asilimia zote.

Akifunga kikao hiki Bi. Haika amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kutunga Sheria Ndogo itakayosimamia utekelezaji wa shughuli za lishe. Pia amewataka Watendaji Kata kupata takwimu sahihi za hali ya lishe kwa maafisa lishe ngazi ya jamii ili ziwasaidie katika kupambana na lishe duni kwenye kata zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.