• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA TATU MANISPAA YA TABORA YAANZA

Posted on: August 30th, 2022

Na Alex Siriyako,

Kamati ya Afya ya Msingi Wilaya ya Tabora imekutana leo hii katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora   na kujadili namna bora ya kuhakikisha Chanjo ya Polio inawafikia walengwa ambao ni watoto walio chini ya miaka mitano kwa awamu hii ambayo ni awamu ya tatu.Hii ikiwa ni utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Utoaji wa Chanjo ya Matone ya Polio awamu ya tatu na zoezi hili litaanza mnamo tarehe 1/9/2022 hadi 4/9/2022.

Kikao cha kamati ya afya ya Msingi kimehudhuriwa na Wajumbe mbalimbali akiwemo mwenyekiti wa Kikao ambae ni Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora, Bi.Haika Masue akimwakilisha Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Paul Chacha, Mhe. Ramadhani Kapera,Mustahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Ndg.Nyahori Mahumbwe,Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora, Viongozi wa Dini mbalimbali,Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na Wajumbe wengine wakiwemo Wataalamu wa Afya.

Polio ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi cha Polio, ambacho huenezwa kwa kula chakula na kunywa maji yaliyo chafuliwa na kinyesi cha mtu mwenye ugonjwa huu. Ugonjwa huu unaweza kumpata mtu kwa kutokuzingatia kanuni za usafi.

Dalili kuu za ugonjwa wa Polio ni Homa, Mafua, Maumivu ya mwili,kichwa na Shingo pamoja na Ulemavu wa ghafla wa Viungo. Watu walioko hatarini Zaidi kupata Polio ni Watoto chini ya miaka mitano(5), ingawa unaweza kuwapata watu wa rika zote.

Ugonjwa huu unaweza kuzuiwa kwa kupata chanjo ya kukinga Polio. Na njia zingine ni kuzingatia usafi wa mikono pamoja na usafi wa mazingira ikiwa ni pamoja na matumizi sahihi ya Choo Bora. Miongoni mwa madhara makubwa ya Ugonjwa huu ni ulemavu wa Kudumu.

Katika hotuba yake kwa wajumbe wa Kamati ya Afya ya Msingi,Bi.Haika amewaasa Wajumbe wote wakawe mstari wa mbele kuelimisha na kuhamasha Umma wa WanaTabora juu ya Umuhimu wa Chanjo ya Polio na madhara ya kutokupata chanjo hii,ili jamii ione kwamba hii ni fursa adhimu katika kupambana na Ugonjwa huu.

Bi.Haika ameeleza kuwa Serikali imechukua hatua hizi za makusudi kufuatia Mgonjwa wa Polio kutangazwa Nchini Malawa mnamo tarehe 17, Februari ,2022,hivyo kutokana na Mwingiliano wa Tanzania na Malawi , Nchi yetu iko kwenye hatari kubwa ya kupata maradhi hayo na hivyo kulazimika kuchukua hatua madhubuti.

Aidha Bi.Haika ameeleza kuwa Manispaa ya Tabora imepokea dozi sitini na tatu elfu(63,000) za chanjo ya matone ya Polio na zimeshasambazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya na ameongeza kuwa Kampeni hii imelenga kuwafikia watoto hamsini na mbili elfu na mia nne themanini na sita (52,486) wenye umri chini ya miaka mitano.

Mwisho kabisa katika majumuisho ya kikao ,Wajumbe waliazimia kwamba Mawakala wa Sensa ya Unwani na Makazi inayoendelea watumiwe kuelimisha Umma kuhusu Polio, Vilevile Viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini, na Taasisi mbalimbali wahusishwe kwa ukamilifu ili kuelimisha Umma na kuleta wepesi wa utekelezaji wa kampeni hii.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.