• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA RASIMU YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: January 18th, 2022

Na Paul Kasembo - TMC.

Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa Tabora kwa kauli moja limepisha Rasimu ya Bajeti  ya Tzs Bilioni 48,921,386,574.89 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya wajumbe wa baraza pamoja na wataalamu wa Manispaa, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nyanja alisema kuwa Manispaa ya Tabora imekadiria kukusanya, kupokea na kutumia kiasi tajwa hapo juu kwa ajili ya mishahara, matumizi ya kawaida na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

“Tumekusudia kufikia kiwango hicho ikiwa ni pamoja na ongezeko la Tzs 366,642.73 ambayo ni sawa na asilimia 6.8 ukilinganisha na bajeti ya 2021/2022 na ongezeko hili limetokana na kukasimia vyanzo vipya vya mapato kwa fedha za miradi ya maendeleo kupitia Ruzuku ya Serikali za Mitaa (LGCDG)” alisema Dkt. Nyanja.

Dkt. Nyanja alisema kuwa, kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri imekusudia kuongeza mapato ya ndani kwa kubuni vyanzo vipya vitano (5) vyenye uhakika na kuimarisha udhibiti wa ukusanyaji wa mapato hadi kufikia asilimia 100.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela alimpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu kwa namna ambavyo ameipatia fedha nyingi Manispaa ya Tabora kwenye bajeti yake kwa asilimia 98 haijawahi kutokea.

Mstahiki Meya pia limpongeza sana Mhe. Rais Samia Suluhu kwa kuipatia Manispaa ya Tabora fedha nyingi za UVIKO-19 ambazo zimewezesha kujenga Vyumba vya Madarasa na Ofisi za waalimu kwa Shule za Sekondari na Shule za Msingi na kukamilika tayari na wanafunzi wameanza kuyatumia tangu tarehe 17/1/2022 shule zilipofunguliwa.

“Nichukue nafasi hii kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu kwa namna ambavyo ameipatia fedha nyingi Manispaa ya Tabora ukianzia kwenye bajeti yenyewe tumepata asilimia 98 jambao ambalo halijawahi kutokea tangu kuanzishwa kwa Manispaa hii, na kwa fedha za UVIKO-19, na sisi Manispaa ya Tabora tunamuahidi nidhamu kubwa zsana kwenye matumizi ya fedha hzio na ushirikiano wa kutosha tutampatia mama yetu”, alisema Mhe. Kapela.

Aidha aliwapongeza sana Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Burian na viongozi wote wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda na viongozi wote ngazi ya Wilaya, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nyanja, Menejimenti, Watendaji wote pamoja na wadau kwa usimamizi na ufuatiliaji wao wa karibu kwenye miradi hii ambapo sasa tumefikia wakati tunajivunia mafanikio hayo yatokanayo ushirikiano wao.

Kando nao, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tabora Mhe. Mohamed Katete pamoja na kuwapongeza Mstahiki Meya wa Manispaa, Waheshimiwa Madiwani, Menejimenti na watumishi wote, lakini pia aliwakumbusha kwenda kusimamia maazimio yote yaliyofikiwa kwenye Baraza ili Manispaa iweze kufikia malengo kama inavyotarajiwa.

 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa mwaka wa fedha 2022/2023 inakadiria kukusanya Tzs 5,451,254,158.28 kwa makusanyo ya vyanzo vya mapato ya ndani.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.