• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA MADIWANI LAMPONGEZA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KWA FEDHA ZA MRADI WA BOOST

Posted on: May 12th, 2023

Na Alex Siriako:

Baraza la Madiwani la Manispaa ya Tabora kwa pamoja limetoa tamko la kumpongeza na kumshukuru Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia S. Hassan kwa kuipatia Manispaa ya Tabora  kiasi cha Tsh.1,893,900,000/= kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, vyoo pamoja na Shule mpya kabisa za Msingi.

Baraza limetoa tamko hili la pongezi na Shukrani leo Mei 12, 2023 katika kikao chake cha Baraza cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Fedha za Mradi wa BOOST kwa Manispaa ya Tabora zinajenga vyumba vya madarasa na vyoo katika Shule za Chemchem ( madarasa 2), Izenga (madarasa 4 na matundu 3 ya vyoo), Kalunde (madarasa 3 na matundu 3 ya vyoo), Kizigo (madarasa 2 na matundu 3 ya vyoo) pamoja na Majengo (madarasa 3 na matundu 3 ya vyoo). Lakini pia fedha hizi zinajenga Shule mpya za Miyemba(mikondo 2), Magereza(mikondo 2) pamoja na Mabatini (mkondo 1).

Pamoja na mambo mengi yaliyojadiliwa, Baraza limejadili taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta zote zilizopo chini ya Halmashauri na kuridhika na kasi ya utekelezaji  wa miradi,ikisimamiwa na timu ya Wataalamu wa Manispaa ya Tabora wakiongozwa na Mkurugenzi wao Dkt. Peter M. Nyanja.

Vilevile Madiwani wameelekeza Halmashauri kupitia Idara ya Mipangomiji ifanye uhakiki wa maeneo yake yote ili yawekwe kwenye mpango wa kuyaendeleza.

Baraza limepokea taarifa ya mapendekezo ya kujenga mabanda ya maduka katika eneo la mjini kati, nyuma ya standi mpya ambapo ndipo wafanyabiashara waliokuwa soko kuu wanapaswa kuhamia na wengine walishahamia tayari. Soko kuu la Mji wa Tabora inatarajiwa kujengwa kisasa kabisa kupitia mradi wa TACTIC. Baraza limepokea na kubariki mapendekezo hayo na kuongeza kuwa utekelezaji ufanyike haraka inavyowezekana.

Aidha Mhe. Ramadhani Kapela, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora amemshukuru sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muunngano wa Tanzania kwa kuendelea kuipatia Manispaa ya Tabora fedha nyingi sana za miradi ya maendeleo na akaongeza kuwa Manispaa ya Tabora ndani ya miaka miwili imetekeleza miradi mingi sana hususani kwenye sekta ya Afya, Elimu na Kilimo kwa Zaidi ya asilimia mia moja ya Bajeti, kitu ambacho toka uhuru hakijawahi kutokea.

Katika kuhitimisha kikao cha Baraza hili, Bi.Neema Kapesa, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora, amewashukuru wajumbe wa Baraza na kuahidi kuwa atatekeleza maelekezo waliyotoa na amepokea ushauri wao kwa heshima kubwa kabisa. Aidha Bi.Neema nae amemshukuru Mhe.Rais kwa kuendelea kuipa upendeleo Manispaa ya Tabora hususani kwenye miradi ya kimkakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.