• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

DC TABORA MJINI AKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA (CHF ILIYOBORESHWA) KWA WATOTO 228 WENYE MAHITAJI MAALUMU TABORA MANISPAA

Posted on: January 22nd, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini Komanya Kitwala leo amegawa Kadi za Bima ya Afya (CHF ILIYOBORESHWA) kwa watoto 228 wenye mahitaji maalumu wanaosoma kwenye Shule za Msingi Viziwi na Furaha zote za Tabora Manispaa.

Kadi hizo za Bima ya Afya zimegharimiwa na shirika la Caritas linalomilikiwa na Kanisa Katoriki Jimbo kuu Tabora ambazo zitaweza kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalumu kupata huduma ya matibabu kuanzia ngazi ya Zahanati mpaka hospitali ya Rufaa popote pale hapa nchini.

Akizungumza wakati wa haflaya kukabidhi kadi hizo kwa wanafunzi hao, Mkuu wa Wilaya alisema kuwa ni vema sasa tuwe na mguso kwa mtu mmoja mmoja, mashirika ya kiserikali au yale yasiyokuwa ya kiserikali kuweza kuwasaidia wanafunzi na wale wasikuwa wanafunzi hasa wale wenye mahitaji maalumu kama hawa ili na wao wahisi wapo kwenye jamii inayowajali na kutambua uwepo wao. Kwa kufanya hivyo kutakuwa na msaada mkubwa sana kwa jamii zetu, serikali na hazina kubwa kwa Mwenyezi Mungu pia.

“Ninawashukuru sana Shirika la Caritas ambalo limejitolea kuwalipia gharama za Kadi hizo zote kwa wanafunzi hawa ambapo leo hii ndiyo nawakabidhi wanafunzi hawa wenye mahitaji maalumu kutoka Shule ya Msingi VIziwi, na Shule ya Msingi Furaha ambayo inafundisha wanafunzi wasioona. Nitumie fulsa hii kuwaomba wahisani wengine yakiwemo mashirika ya kiserikali na yasiyokuwa ya kiserikali kuiga mfano huu wa shirika la Caritas, aidha nimshukurui pia Afisa Maendeleo ya Jamii wa Manispaa ya Tabora Tumaini Mgaya ambaye alishiriki kuandaa kazi hiyo yote.” Alisema Komanya.

Kwa upande wake Sheikh wa Wilaya ya Tabora Mjini Ramadhani Juma alimshukuru sana Mkuu wa Wilaya kwa kutambua uwepo wake na hata akamualika kwenye hafla hiyo, pia akatumia fulsa hiyo kuwapongeza Caritas kwa namna walivyoguswa hata wakaamua kugharamia kadi hizo za Bima ya Afya. Kisha akatumia fulsa hiyo kuwaomba wahisani wengine kuweza kujitokeza kuwasaidia watoto hasa wenye mahitaji maalumu waweze kuhisi kuwa tupo pamoja, maana kwa hali waliyonayo kwa sasa ni kama yatima vile, hivyo tushirikiane kuwasaidia na tusiwaachie peke yao shule husika klwa hao watoto ni wetu sote.

Naye Mch. Marco Ngalu wa Kanisa la AICT TABORA, aliwapongeza sana wadau wote akianzia na Mkuu wa Wilaya kwa namna ambavyo amekuwa akisaidia shughuri nyingi za kijamii ikiwemo hii ya leo ya kukabidhi kadi za bima ya afya kwa wananfunzi hawa wenyewe mahitaji maalumu wa Shule hizi za Msingi Viziwi na Furaha. Lakini pia alitumia fulsa hiyo kuwaomba wadau wengine mbali mbali waweze kujitokeza kuwasaidia wanafunzi hao ambao kwakweli wanahitaji ukaribu zaidi muda wote.

Kukabidhiwa kwa kadi hizo kwa wanafunzi hao wa shule za msingi Viziwi na Furaha kutawapatia uhakika wa matibabu ya afya na hivyo kuwawezesha kusoma na kwa uhakika na hatimae kuongeza ufaulu zaidi kwakuwa watakuwa na afya njema wakati wote.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA (PSLE) 2020 November 21, 2020
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 MANISPAA YA TABORA December 18, 2020
  • Usafi wa Mazingira kwa Wananchi Wote, Jumamosi ya mwisho kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI MANISPA YA TABORA LAPITISHA MAPENDEKEZO YA BAJETI YA BILIONI 50.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022

    February 13, 2021
  • DC KOMANYA AZINDUA SHUGHURI ZA UHAMASISHAJI WA BIMA YA AFYA YA JAMII (CHF ILIYOBORESHWA) MANISPAA YA TABORA

    January 19, 2021
  • MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI KIFUA KIKUU NA UKOMA WADHAMIRIA KUZIFIKIA KATA ZOTE TABORA MANISPAA

    December 18, 2020
  • MSTAHIKI MEYA TABORA MANISPAA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA VILEO

    December 17, 2020
  • Angalia Zote

Video

MSTAHIKI MEYA BW. RAMADHAN KAPELA - UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NA UWEKEZAJI KATIKA MANISPAA YA TABORA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA
  • Taarifa Mbalimbali
  • Fomu ya maombi ya Leseni
  • Jarida 2020
  • Taarifa kwa Umma
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Manispaa Tabora - Barabara ya Boma

    Anwani ya Posta: S.L.P 174 Tabora

    Simu ya Ofisi: 026-2604315/6088

    Simu ya Mkononi: 0786820518

    Barua Pepe: md@taboramc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.